Karagwe
Zaid ya Migomba 463,000 imengolewa katika wilaya ya Karagwe na Kyerwa kutokana na ugonjwa wa myauko bakteria unaoshambulia migomba
katika kipindi cha mwaka 2006/2013.
Kauli hiyo imetolewa jana na kaimu Afsa kilimo wa wilaya ya karagwe
Dominic Eustad wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
Eustadi alisema kuwa migomba 463.000 imeishangolewa
katika kata 40 za wilayani hiyo kutokana
na kuathirika kwa ugonjwa mnyauko bakteria unaoathiri migomba ambapo alisema
kuwa migomba iliyoathirika ni 764,492 na
kaya zilizoathirika ni 31,963 kati ya kaya 108,301 za Wilaya hiyo.
Alisema kuwa ugonjwa huo uliingia kwa mara ya kwanza
mkoani kagera katika wilya ya Muleba kata ya Izigo mwaka 2006,na kuwa katika
wilya ya karagwe mnyauko huo ,uliingia katika kata za Murongo,na Kibingo
Wilayani Kyerwa kutokea nchini Uganda.
Alisema ugonjwa huo
unaenezwa kutokana na vifaa vya mashambani,wadudu,Ndege ,Wanyama na kuwa kila kaya inalazimika kutumia vifaa
vyake na kuongeza kuwa Ugonjwa huo hauna
dawa ya kutibu au kuzuia kuenea.
Alisema kuwa katika udhibiti wa ugonjwa huo,Ofsi
yakeinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na mashamba makubwa
kukanda na kuchangia katika uenezi wa
mashamba yenye kesi na yaliyotelekezwa
na baadhi ya mashamba ya wazee.
Alisema mkulima ambaye atakayekiuka sharti lililoainishwa katika
kifungu cha 7(1)c) cha sheria ndogo atakuwa ametenda kosa na atawajibika kulipa
faini kwa Afsa mwidhini au Afsa ugani shilingi 10,000 kwa kila mgomba ambao
atashindwa kuukata na kuuzika ili asiambukize ambayo bado haijaambukizwa.
Aidha alisema kuwa dalili za ugonjwa huo ni pamoja na
majani ya mgomba kubabuka,tunda la mgomba kuiva kabla ya wakati ,ua dume
kunyauka na kwenye shina kutoa utomvu ulioganda.
Hata hivyo amesema wanasiasa wameanza kuelewa zoezi
hilo na kuhamasika kwa kuwaunga mkono maafisa ugani katika udhibiti wa ugonjwa
huo ambapo aliongeza kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu wa maafsa ugani.
No comments:
Post a Comment