Tuesday, August 18, 2015

WITO WATOLEWA KWA WANAOHITAJI UONGOZI MWAKA HUU.


Na Juhudi  Felix-KARAGWE

Paroko wa parokia ya Kabanga  jimbo katoriki la Kigoma  padre John Babitisit  Mapunda  ameishauri  Taasisi ya kuzia na kupambana na rushwa  TAKUKURU kuwachukulia hatua  wanaokiuka maadili ya uchaguzi katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Ushauri huo ameutoa wakati akizungumza na Radio Fadeco kwa njia ya simu,Agost 17 mwaka huu,na kusema kuwa TAKUKURU haina budi kutumia sheria kuwabana wanaotumia fedha kupata madaraka kwani rushwa katika uchaguzi inaathiri mfumo wa utoaji haki katika Nyanja za za siasa, uchumi na mazingira.

Mapunda amesema kuwa Rushwa kwa wakristo ni dhambi ambapo inasababisha kudidimiza uchumi wa Nchi na wanao husika katika kutoa na kupokea rushwa  lazima   wathibitiwe.

Amedai kuwa Rushwa kwa sasa inaoneka kuwa ugonjwa wa ambao hauponi ,badala ya kupungua inaongezeka kupitia Viongozi ambao wange kuwa watendaji wakuu katika  kukomesha vitendo hivyo.

Amewataka waumini wa madhehebu mbalimbali hapa nchini wasiburuzwe na wanasiasa bali waijue siasa kwa kutumia akili waliyopewa na Mungu kwani  hakuna dini inayokubali watu wake wawe maskini katika suala la maendeleo na kuwataka wabadilike  kwa kuzisoma harama za Nyakati.

Aidha amesisitiza watanzani kutambua madhara yatokanayo na Rushwa katika unyanyasaji kimaendeleo kwa kutumia sanduku la kura kuleta mabadiliko katika nchi  kwa kuwa na utawala bora.

Hata hivyo Mapunda ameongeza kuwa  Tume ya Taifa  ya Uchaguzi NEC ihakikishe inaweka nguvu zote kurekebisha kasoro za vitambulisho  vya wapiga kura ili itendeke haki kwa wote katika kupiga kura muda utakapo wadia.

1 comment: