Saturday, December 12, 2015

BODABODA WATAKA ELIMU YA USALAMA BARABARANI ITOLEWE KWA WATUMIA VYOMBO VYA MOTO.BOFYA HAPA


Waendesha  pikipiki maarufu kama bodaboda wameiomba serikali kutatua changamoto wanazokumbana nazo  pamoja na kuwapunguzia faini wakati dreva anapokuwa na kosa kwani kipato chao ni  kidogo wanachopata kutokana  na  kazi  hiyo.

Hayo yamesemwa na baadhi ya waendesha bodaboda Disemba12 mwaka huu ambapo wamesema kuwa miundombinu ya barabara imekuwa changamoto kubwa kwao kwani kuna sehemu ambazo barabara ni mbaya, ikiwemo na  kupunguziwa faini kulingana na kosa mtu analokuwa nalo kwani wamekuwa wakitozwa faini ya kiasi cha pesa ambacho nikikubwa na kipato chao kiko chini sana.
   
Naye mwenyekiti msaidizi wa waendesha pikipiki Fashiru Abdul amesema kuwa anaiomba serikali iendelee kutoa elimu kwa watumiaji wa pikipiki kwani kumekuwa na watu wanaoendesha pikipiki bila kujua sheria za barabarani na kusababisha ajali  kwa sababu ya kutokuwa na elimu juu ya uendeshaji wa pikipiki pamoja na sheria za barabarani.
                              
Aidha Abdul amewaomba waendesha pikipiki kuwa makini barabarani na kupunguza  mwendo kasi katika kipindi hiki cha sikukukuu kwani  kuna msongamano mkubwa wa watu ili kuweza kujiepusha na ajali.

No comments:

Post a Comment