Kijana mmoja Wa Mtaa wa Muleba Mjini Wilayani Muleba
aliyejulikana kwa jina la Muta Mtalemwa Aliyekadiriwa kuwa na umri wa miaka
kati ya 22 na 23, Ameuawa Kwa kupigwa na Nondo Kichwani usiku wa kuamukia leo.
Kifo hicho kimempata wakati alipokuwa akitoka kwa Baba yake
Mkubwa akielekea kwa Baba yake ndipo watu wasijulikana walipomvamia na kumpiga
na nondo kichwani.
Akizungumuza na KARAGWE FORUM Mwenyekiti wa Mtaa huo Panckrasi Mtwara amesema kuwa Mara baada ya
kijana huyo kuvamiwa alikimbizwa Hospitalini kwa ajili ya kupatiwa Matibabu na
kuwa baada ya muda wa saa moja hali yake ilibadilika kufikia alfajili
ya leo kijana huyo alikata roho..
Aidha, Mtwara ameongeza kuwa Mpaka hivi sasa waliohusika
na tukio hilo bado hawajafahamika ingawa vyombo vya ulinzi na usalama
vinaendelea na Uchunguzi ili kuwabaini waliohusika huku akiwataka wananchi kuwa
wapole katika kipindi hiki kigumu..

No comments:
Post a Comment