Wakati wakristo
na wananchi wote
kwa ujumla wakiendelea
na shamrashamra za
kusherekea kumbukumbu ya
kuzaliwa Yesu Kristo
ijulikanayo kama NOEL
au Krismansi mtu
mmoja mkazi wa
kijiji Cha Nyakayanja kata
ya Nyaishozi amekutwa
bafuni amefariki dunia.
Aliyekutwa amefariki
ametambuliwa kwa jina la
Joseph Kaneganega ambaye alikuwa
akifanya kazi za
ulinzi kijijini hapo amekutwa
bafuni wanapofanya kazi hali
iliyopelekea taarifa kutolewa
kwa uongozi wa
kijiji.
Taarifa za
awali zimebainisha kuwa marehemu
Joseph Kaneganega amekutwa
na mabaki ya
pombe ya kienyeji
na gongo ya
kienyeji kwenye chupa
za plastiki.
Wakati huo huo mkazi mwingine atumia pombe na kuzidiwa hali iliyopelekea kukurogewa kilogramu mbili za sukari na kuzinywa hali iliyomfanya azinduke.
Afisa mtendaji wa kata
Nyaishozi,Nickolausi Burukadi Kachencha
wakati akiongea na wananchi wa maeneo hayo
Desemba 25 mwaka huu,amewaomba wananchi wa Nyakayanja na Mtakuja kupunguza unywaji wa pombea aina ya
Viroba eti wakidai kuwa wanasherekea
sikukuu ya Noel.
Mtendaji huyo amezungumza
hayo kutokana na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Kalingo Amosi mkazi wa
kitongoji Mtakuja kijiji Nyakayanja baada ya kunywa pombe nyingi kuzidi kiasi .

No comments:
Post a Comment