Sunday, January 10, 2016

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU SHUGHULI ZA UVUVI KWA KIPINDI CHA MIEZI SITA WANANCHI WALALAMIKA


Serikali  ya  wilaya  ya  Karagwe  imetoa  muda  wa  mwezi  mmoja  kwa  wananchi   wilayani  Karagwe  kujiandaa  kusitisha  shughuli  za  uvuvi  wa  samaki  kwenye  maziwa  yote  yanayopatika  ndani  ya  wilaya  kwani  kuanzia  mwezi  wa  pili  shughuli  zote  za  uvuvi  zitasitishwa  kwa  kipindi  cha  miezi sita.

Agizo  hilo  limetolewa  leo  na  mkuu  wa  wilaya  ya  Karagwe  Deodatus  Kinawiro  katika  kikao  cha  wadau  wa  maendeleo  kilichojumuisha  viongozi  wa  dini,mashirika  ya  kiraia,wananchi  na  wataalamu  mbalimbali  wa  halmashauri  ya  wilaya  ya  Karagwe.

Kinawiro  amesema  awali  walitangaza  shughuli  zote  zingesitishwa  kuanzia  Januari mosi  mwaka  huu  lakini  kuna  malalamiko  yalitolewa  na  wananchi  kuwa  imekuwa  ghafla   na    hawakupewa   muda  wa  kujiandaa  hivyo  wamesikiliza  malalamiko  hayo  na  kutoa  fursa  hiyo  ya  kujiandaa.

Amesema  ratiba  ya  kusitisha shughuli  za  uvuvi  kwenye  maziwa  yanayopatikana  kwenye  wilaya  ya  Karagwe  itakuwa  ya  kudumu  kila  mwaka  kwa  kipindi  cha  kuanzia  januari  hadi  mwezi  wa  sita

Hata  hivyo  ametoa  onyo  kwa  wananchi  kutotumia  kipindi  hiki  cha  kujiandaa   kinyume  na  taratibu  na  sheria  zinavyotakiwa  vinginevyo  atakayebainika   sheria  dhidi  yake  zitachukua  mkondo  wake.

No comments:

Post a Comment