Friday, March 2, 2012

AJIRA SI SERIKALIN INAWEZEKANA KUJIAJIRI





Ajira  si mpaka serikalini   au kwenye taasisi   kumbe kuna fursa nyingine za kujiajiri ili kuweza kujipatia kipato cha kukidhi mahitaji yako.Hapa ni Bwana Elias Zakaria 25 ambaye ni mwanakikundi cha BUDAP ambacho kinafanyia shughuli zake KIROYERA TOURS ambayo ni kampuni ya utalii inayojihusisha na utunzaji wa utamaduni wa mkoa wa Kagera.

BUDAP  ni kikundi cha walemavu ambacho kilianzishwa mwaka 2005 kinajihusisha na kazi za mikono  kama vile utengenezaji wa vifaa vya muziki asilia  kama vile ngoma za asili,malimba,na ufundi wa kushona nguo kwa kutumia cherehani.Bwana Elias   anabainisha kuwa walianza wakiwa wanakikundi zaidi ya kumi lakini kwa sasa wamebakia wanakikundi sita ,mmoja ni wa kike na watano ni wanaume

Alisema kuwa moja ya sababu zilizochangia  kupunguza wanakikundi  kuwa baadhi yao walipopata ujuzi waliamua kwenda kuanzisha vikundi ama kufanya shughuli zao binafsi.Akibainisha mafanikio wanayopata ni kuwa wanapata kipato cha kukidhi  mahitaji yao kwa kuuza vifaa hivyo kwa wageni wanaofika kutembelea makumbusho hayo

Hii inaonesha  kuwa tusiwe tunawanyanyapaa walemavu kwa mtazamo wa baadhi ya watu katika jamii kuwa na dhana potofu  ya kuwaona watu wenye ulemavu hawawezi kufanya kazi yoyote kumbe inawezekana wakipewa ushirikiano wa kutosha na kuondoa  unyanyapaaji.










No comments:

Post a Comment