NA
JUHUDI FELIX
KAYANGA
-KARAGWE
Askari
jeshi mstaafu ,raia wa nchi ya uganda Luten Bashiru Karimunda miaka
40,amehukumiwa kwenda jera miaka 2 katika wilaya karagwe kwa kosa la kuingia
nchini bila kibali.
Mbele
ya hakimu wa mahakama hiyo Peter Matete mwendesha mashitaka wa polisi
Juma Lipwata ameeleza mahakamani hapo kuwa mshitakiwa aliingia nchini
Tanzania tarehe isiyojulikana Oktoba 2012 akitokea nchini Uganda ,na alifikia
katika kijiji cha Rwabigaga kata Mabira wilaya mpya ya Kyerwa bila kuwa na
kibali.
Awali
mshitakiwa nchini Uganda alikuwa askari mstaafu wa jeshi la nchi hiyo mwenye
Namba RO 5788 na mnamo mwaka 2012 alipewa cheo cha Luteni katika jeshi la
UPDF,mshitakiwa ni mkiga na wazazi wake wote ni raia wa nchi hiyo.
Imedaiwa
mahakamani hapo kuwa mshitakiwa mnamo Februaly 27 mwaka huu akiwa Kyerwa
aliwekwa chini ya ulinzi na kupelekwa ofsi ya uamiaji Murongo,na mnamo MOSI
March mwaka huu mshitakiwa alipelekwa
katika ofsi ya uhamiaji Karagwe,na badaye machi
4 mwaka huu mshitakiwa alifikishwa mahakamani.
Kwa
upande wake mshitakiwa alijitetea na kuomba mahakama imsamehe kwani alifika nchini humo kuhudhuria kesi ya
Ardhi yake ambayo ilidhurumiwa na pia ameongeza kuwa kwa sasa ni mgonjwa ambapo
anatembelea magongo baada ya kupata maumivu katika mguu wake wa kulia.
Hata
hivyo mshitakiwa amehukumiwa kwenda jera
miaka miwili baada ya hakimu wa mahakama hiyo kuridhika na
ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka .
Akitoa
hukumu hiyo Matete amesema kuwa ametoa adhabu hiyo kali ili iwe fundisho kwa
wahamiaji wote wasio kuwa na vibari vya kuingia na kutoka nchini.
No comments:
Post a Comment