Friday, March 2, 2012

KARAGWE KATIKA MABADILIKO.

 

 

 

 

RISALA YA UZINDUZI WA MIAKA HAMSINI (50) YA UHURU WILAYANI KARAGWE TAREHE 04/11/2011 /20

1.UTANGULIZI.
Mh.Mgeni Rasmi,
Ninachukua nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwako kwa kukubali wito wakuungana nasi katika sherehe hii ya uzinduzi wa Miaka Hamsini (50)ya Uhuru Wilayani Karagwe sambamba na Sikukuuu ya Wakulima Nane Nane Mwaka 2011.
 
1.1 HALI YA WILAYA KWA UFUPI
Wilaya ya Karagwe ni kati ya Wilaya 8 za Mkoa wa Kagera .inapatikana katika Latitude nyuzi 1º hadi 20º Kusini ya Ikweta na Longitude 30º hadi 38º. 30” Mashariki mwaGreenwich . Wilaya inapakana na Nchi ya Uganda upande wa Kaskazini, Nchi ya Rwandaupande wa Magharibi, Wilaya ya Ngara upande wa Kusini na Wilaya ya Misenyi na Mleba upande wa Mashariki. Mto wa Kagera upo mpakani mwa Wilaya ya Karagwe na Nchi ya Rwanda na sehemu ya Kaskazini Magharibi mwa Nchi ya Uganda .
 
Wilaya ina eneo la Kilimita za Mraba 7,716,kati ya hizo Kilomita za Mraba 7,558 ni eneo la nchi kavu na Kilomita za Mraba 158 ni eneo la maji. Mwinuko wa Ardhi kutoka usawa wa Bahari ni Mita 1500 hadi Mita 1800. mwinuko mrefu ni Mlima wa Rwabunuka .Hali ya hewa kwa ujumla ni joto la wastani wa 20- 26ºC. Mvua zinanyesha kwa wastani wa Milimita 1,040 hadi 1,200 kwa Mwaka kati ya Mwezi September na Januari na kati ya Mwezi Machi na Mei.
 
1.2  UTAWALA
Kiutawala Wilaya imegawanyika katika Tarafa 9, Kata 40 Vijiji 166 na Vitongoji 1,373. Katika mgawanyiko huu, Tarafa 5 Kata 12 Vijiji 57 na Vitongoji 211 ni vipya. Tangu Mwezi Julai 2010 Serikali iliridhia ombi la kuanzisha Wilaya mpya ya Kyerwa, iliyo na Tarafa 4 Kata 18, Vijiji 93 na jumla ya Vitongoji 646. Tunayo majimbo 2 ya uchaguzi ya Karagwe na Kyerwa yaliyo na Wabunge wafuatao:-
- Jimbo la Karagwe- Mhe.Gosbert Blandes (CCM)
- Jimbo la Kyerwa- Mhe. Eustace.O.Katagira(CCM)
 
 
 
 
1.3  IDADI YA WATU
Kwa mjibu wa Sensa ya Mwaka 2002 Wilaya ilikuwa na watu 423,423.
(Me 207,850 na Ke 215,573). Ongezeko la watu kwa Mwaka ni Asilimia 2.9. Hivyo inakadiliwa kwa kutumia ongezeko hilo Mwaka 2011 Wilaya ilikuwa na idadi ya watu wapatao 639,651.
 
2. HISTORIA YA WILAYA
Wilaya ya Karagwe ilizinduliwa Mwaka 1958 na Gavana Richard Turnbull baada ya kumegwa kutoka katika Wilaya ya Bukoba. Kwa hali hiyo Wilaya ya Karagwe ilikuwepo wakati Tanganyika inapata Uhuru wake hapo tarehe 9/12/1961. Wakati huo shughuli za kiutawala zilikuwa zinafanyika katika maeneo mawili tofauti yahani Kayanga na Nyakahanga (yaani Ahalukiko). Baadae Kayanga ikawa ndiyo Makao Makuu ya kiutawala ambako Mkuu wa Wilaya alikuwa akifanya kazi wakati huo Nyakahanga palikuwa panatumiwa na Omkama kama Makao Makuu yake.
 
Kabla ya Uhuru kulikuwa na utawala wa Ma-chifu (Omukama) na Mabaraza yaliyojulikana kama Gombolola. Chifu (Omukama ) alisaidiwa na Katikiro ambaye alikuwa msaidizi wake Mkuu. Chini ya uongozi wa Katikiro walikuwepo wasaidizi waliojulikana kama Abakungu. Kazi ya Abakungu ilikuwa ni kuhakikisha amani na usalama vinakuwepo kusimamia na kuhimiza maendeleo na kutoza kodi ya kichwa.
 
MUUNDO WA WILAYA WAKATI WA UHURU NA JINSI ULIVYOBADILIKA
Wakati wilaya inaanza waka 1958 ikuwa imegawanyika katika maeneo ya utawala yaliyokuwa yanajulikana kama “subchiefs”. Haya maeneo yalikuwa 7 nayo ni
Bugene – palijulikana kama migongo
Nyaishozi – palijulikana kama kiyanja
Nyabiyonza – palijulikana kama chikuba
Kituntu – palijulikana kama bugabwe
Mabira – palijulikana kama marungu
Kaisho – palijulikana kama buganga (karagwe keifo)
Murongo- palijulikana kama buganga
 
Kila “subchief” ilikuwa na kiongozi wake aliyefahamika kama mwami wa gombolola ambaye alifanya kazi chini ya chifu (omukama wa karagwe).
 
Mwaka 1965, “subchiefs” hizo ambazo baadae zilikuja kuitwa kata zilizoongezwa na kuwa 28 hadi mwaka 2010 nazo ni bugene ihanda nyakahanga kiruruma bweranyange kibondonyakakika  kayanga ndama rugu nyakasimbi ihembe nyaishozi nyabiyonza kihanga kituntu igurwa mabira kimuri kamuri rwabwere nkenda kaisho isingiro murongo kyerwa kibingo na  bugomora.
 
Watu wenye uhalifu mdogo na wenye kesi za migogoro ya ardhi walikuwa wanahukumiwa kwenye “subchiefs” hizo. Wenye kuhusika na mauaji na kesi za mogogoro ya ardhi walipelekwa bukoba ambapo omukama alihukumu kesi/mashauri yaliyowashinda abakungu.
 
Na pia ziliundwa tarafa 4 ambazo ni
Bugene/nyaishozi
Nyabiyonza
Kutuntu/mabira
Kaisho/murongo
Baada ya baraza kuvunjwa na machifu  kuondolewa,wilaya ilipata  mkuu wa  wilaya  wa kwanza  mwananchi  aliyeitwa  ndugu  Peter Kafanabo  mwaka  1961.Pia alikuwa katibu wa  kwanza wa  TANU Karagwe.
 
Halmashauri  ya  wilaya  ya  Karagwe ilaundwa  mwaka  1965 wakati  huo  ikiwa inajulikana kama  Buhaya district council hadi mwaka 1872 chni ya uenyekiti wa ndugu Ferdinand Mujungu. Baada ya hapo ilivunjwa na kuwa “district development council” hadi mwaka  1984. mwaka 1984 ndipo ilipoundwa Halmashauri hii ilipo sasa. Tangu  wakati huo wenyeviti wake wamekuwa kama ifuatayo:-                                                                                                                 
     
       1.ndugu H.N Kyakatuka                   1984-1988.
       2.ndugu Salvatory Kalabamu           1989-2005.
      3.ndugu S.R kashunju                        2006-mpaka sasa.
     
    Pia wakurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Karagwe tangu ianzishewe mwaka 1984 ni kama ifuatavyo:-
1.Ndugu G.E. KAgaruki                 1984-1986
2.Ndugu E.J. Muganda                   1986-1989
3.Ndugu T.K. Ndibarema                1989-1992     
4.Ndugu O.K. Mwasha                    1992-1998
5.Ndugu S.A Masindike                  1998-2002
6.Ndugu M.S. Mboje                       2002-2006
7.Bibi C.M. Kamuhabwa                 2006-2010
8.Bwana  E Kahabi (Kaimu)            2010 hadi sasa
 
 
HALI YA UONGOZI TANGU 1961
            Wilaya ya Karagwe imewahi kuwa na uongozi wa wakuu wa wilaya kama ifuatavyo:-
1.Marehemu PETER N. KAFANABO            1961-1965
2.Marehemu ENOS RYANGARO                  1965-1969
3.Ndugu LOSA LIYEMBA                              1969-1973
4.Ndugu THOMAS MSONGE                          1973-1977
5.Ndugu RUHASI                                              1977-1978
6.Lt. F.X.ITALA                                               1978-1980
7.Ndugu RAPHAEL CHAYEKA                     1980-1984
8.Marehemu MOHAMED CHAMSALA          1984-1989
9.Ndugu LUHOZYA E.SIWALE                       1984-1989
10.Capt. JOSEPH E. NDITI                                1989-1997
11.Ndugu GERARD J.GHACHOCHA              1997-1999
12.Ndugu PETER KANGWA                             1999-2000
13.Ndugu SANGO OLETELELE                       2000-2004
14.Ndugu DAVID J. DAUD                                2004-2006
15.Ndugu FRANK UHAHULA                           2006-2009
16.Col.Mst FABIAN I.MASSAWE                     2009hadi sasa
              
MATUKIO NA MABADILIKO MAKUU KISIASA, KIUCHUMI, KIUTAWALA, KIULINZI, KITEKNOLOJIA NA KIJAMII.
a)     KISIASA
Wilaya ya karagwe ilianzishwa mwaka 1958 chini ya utawala wa wakoloni. Mabadiliko ya kwanza kisiasa yalikuwa ni yale ya utawala kutoka kwa wakoloni kwenda kwa wananchi wenyewe kupitia uhuru wetu wa mwaka 1961. aidha viguvugu la mfumo wa vyama vingi vya siasa lilianza mapema katika harakati za kutaka kujitawala kutoka kwa wakoloni wa kiingereza na utawala wa kifalme wa kiarabu vyama hivyo ni TANU TAA AFROSHIRAZ PARTY. Baada ya uhuru uongozi wan chi ulikuwa chini ya chama kimoja cha TANU na baadaye CCM. Mabadiliko ya sasa ni utawala wa vyama vyingi vya siasa vilivyosajiliwa ni CCM,CHADEMA,CUF,TLP,na NCCR Mageuzi. Mwenyekiti  wa kwanza wa TANU alikuwa Bwana Kahungya. Waliofuatia tangu wakati huo ni kama ifuatavyo:-
1.     Ndugu Eliakim Kahungya
2.     Ndugu Martin Pancras
3.     Ndugu Fredinand Majungu
4.     Ndugu Hezekiel Kyakatuka
5.     Ndugu Gregory Rwabutomize
6.     Capt.Salvatory Rwechungura
7.     Ndugu Audax Kagaruki
8.     Ndugu Justinian Kazungura 2007 hadi sasa.
 
Aidha Wilaya ya Karagwe iliwahi kuwa na Wabunge wafuatao:-
JINA                                                                     MWAKA                      JIMBO
1.     Mheshimiwa Gervase Kaneno                  1965 – 1968                  Karagwe
2.     Mheshimiwa Laurent Nyamalaba             1968 – 1975                 Karagwe
3.     Mheshimiwa Venant Rwabuti                   1975 – 1980                 Karagwe
4.     Mheshimiwa Elikano Byeitima                  1980 – 1995                Karagwe
5.     Mheshimiwa Sir George Kahama               1995 – 2005                Karagwe
6.     Mheshimiwa Eustace O.Katagira                1995 – 2000               Kyerwa
7.     Mheshimiwa Mtungirehi                              2000 – 2005               Kyerwa
8.     Mheshimiwa Gosbert Blandes                      2005 – hadi sasa       Karagwe
9.     Mheshimiwa Eustace O.Katagira                 2005 – hadi sasa        Kyerwa
 
b)    KIULINZI
Kabla ya kupata uhuru mwaka 1961, ulinzi wilayani karagwe ulikuwa ni ule wa jadi.baadae mgambo, askari polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama viliongezwa. Mwaka 1978/1979 sehemu ya wilaya ya karagwe ilikuwa miongoni mwa maeneo yaliyovamiwa na majeshi ya Uganda sehemu ya mpakani mwa Tanzania na Uganda . Kati ya mwka 1993 na 1994, wilaya ilikumbwa na wimbi la wahamiaji haramu kutoka nchi ya Rwanda ambao walikuwa wanakimbia mauwaji ya kimbari. Wahamiaji haramu haao walifuata njia zilizopitiwa na Ndugu zao mwaka 1957 – 1962 ambao pia walikuwa wanakimbia vita vya kikabila.
 
Athari za matukio haya:-
a)     vita vya kagera iliathiri hali ya maendeleo hasa katika sehemu za mpakani katika kata za mrongo, Bugomora na kibingo.
b)    Wimbi la wahamiaji haramu lilipelekea kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu na uharibifu wa mazingira. Mifugo (ng’ombe) waliibiwa kutoka wilayani kwenda nchi jirani za Uganda na Rwanda kwa wingi maeneo mengi ya karagwe yalianza kukaliwa na wahamiaji haramu. Nafasi za masomo nyingi hasa shule za msingi zilijazwa wahamiaji haramu, hata nafasi za kazi za maofisini na katika sekta ya afya nazo zilijazwa na wahamiaji haramu. Hata baada ya nchi za Uganda na Rwanda kuwa na amani na usalama wimbi kubwa la wafanyakazi waliosomeshwa na taifa hili walihamia katika mataifa yao na kuacha pengo la kiutumishi Tanzania
 
c) KIUTAWALA
Mwaka 2011 mabadiliko makubwa yaliyotokea na serikali kuridhia mgawanyiko wa wilaya kutoka kuwa moja hadi kuwa mbili yaani wilaya ya karagwe  na wilaya ya kyerwa. Aidha mabadiliko yafuatayo yametokea baada ya mgawanyiko wa wilaya ya karagwe.
Tarafa zimeongezeka toka 4 za awali hadi 9 za sasa
-kata zimeongezwa kutoka 28 hadi 40
-vijiji vimeongozwa toka 109 hadi 166
- mamlaka ya mji mdogo wa kayanga imeanzishawa
-waheshimiwa madiwani wa kata mpya walichaguliwa kata uchaguzi mkuu wa mwaka 2011.
 
d)  KIUCHUMI
Mabadiliko makubwa yaliyotokea kuichumi ni pamoja na kupanuka kwa kilimo ambacho ndiyo shughuli kuu ya kiuchumi ya wananchi wa karagwe. Uzalishaji wa kilimo kwa mazao kama ndizi, mahindi, maharage viazi matunda kahawa n.k. umeongezeka kulingana na kipindi nchi yetu inapata uhuru mwaka 1961. aidha kabla ya uhuru madini ya TIN yalikuwa yanachimbwa huko kyerwa. Uchimbaji huo kwa sasa umebakia kwa wachimbaji wadogowadogo tu. Wakati huo umeme wa kutumia nguvu za maji (HEP)ulizalishwa kutoka kwenye maporomoko mya mto kagera eneo la mrongo hadi kyerwa “syndicate” kwa ajili ya kuchimba kusafisha na kubagua TIN. Mitambo hiyo ya umeme iliharibiwa na Idd Amin wakati wa vita vya kagera 1978 – 1979 .
 
Hali ya maaendeleo kiuchumi imekuwa kubwa kwa upande wa kilimo kwani uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara hasa kahawa umeongezeka. Kukua huku wa uchumi kumeenda sambamba na kuongezeka kwa watu hususani wahamiaji kutoka wilaya zingine za bukoba muleba biharamulo na ngara.
 
a)     KITEKNOLOJIA
Wakati Tanganyika inapata uhuru mwaka 1961 hali ya maendeleo ya kiteknolojia wilayani karagwe ilikuwa duni. Kwa sasa hali imekuwa tofauti kuna umeme, kuna mawasiliano ya simu za mezani na mkononi, kuna matumizi ya computer na internet n.k. umeme uliokuwepo kabla ya uhuru ulitoka kikagati  Uganda na kwenda kyerwa kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya bati (TIN). Umeme huo uliondolewa baada ya machimbo hayo kufungwa na matokeo ya vita vya kagera.
b)    KIJAMII
Wakati Tanganyika inapata uhuru, wilaya ilikuwa na huduma chache za kijamii zilizokuwa zikiwafikia watu wachache. Kwa mfano:-
·        Kulikuwa na shule chache sana za msingi lakini pia kulikuwa na shule zilizokuwa zikijulikana kama middle schools nazo ni lukajange nyaishozi bugene rwambaizi shule ya kwanza ya sekondari kuanzishwa wilayani karagwe ilikuwa karagwe sekondari iliyoanzishwa mwaka 1977 na kanisa la kilutheri na ilianzia katika majengo ya rukajange middle school.
·        Kulikuwa na zahanati tatu nyakahanga isingiro na nyakaiga ambazo zote zilikuwa zikimilikiwa na madhehebu ya dini.
·        Mawasiliano ya simu hayakuwepo hususani simu za viganja
·        Umeme ulioenea sehemu kubwa ya wilaya haukuwepo umeme wa sasa uliletwa baada ya vita ya Tanzania na Uganda na hasa katika kipindi cha utawala wa rais Mseveni
·        Huduma ya maji safi na salama iliwafikia watu wachache walioishi mjini kayanga na omurushaka.
 
1.     MAFANIKIO YALIYOPATIKANA TANGU UHURU HADI SASA 
a)     Elimu
 Shule zimeongezeka sana na hadi sasa wilaya ina shule za msingi 212 na sekondari 48. kuna vyuo viwili vya ualimu ambavyo vinaendelea kujengwa na pia kuna mpango wa kujenga chuo kikuu cha kilimo chini ya kanisa la kiinjili la kilutheri .
 
b)    afya
wilaya ina zahanati 50,kati ya hizo 38 ni za serikali na zilizobaki ni za binafsi. Vituo vya afya vipo 5,vinne vya serikali na kimoja cha shirika la dini
 
c)     mtandao wa barabara za wilaya umeimalishwa na kwa sasa una jumla ya km. 518.7,tabaka la lami nyepesi ni km 13 (kutoka mugakorongo hadi nyakahanga Hospital) barabara za tabaka la udongo ni km. 384. barabara kutoka kyaka hadi bugene yenye urefu wa km.59 inajengwa kwa kiwango cha lami hivi sasa.
 
d)    kuna huduma za uhakika za mawasiliano ya simu
 
e)     kuna huduma ya umeme katika baadhi ya maeneo ya wilaya
 
f)      kuna radio za jamii za FADECO na radio karagwe ambazo zimesaidia jamii kupata habari elimu na burudani.
 
g)     Upatikanaji wa mafuta aina zote na vyombo vya usafiri na usafirishaji wa uhakika ambao umewezesha uchumi wa wilaya kukua kwa kasi.
 
h)    Uzalishaji wa mazao ya kilimo na biashara umeongezeka ukilinganisha na watu wa uhuru.
 
2.      
3.     CHANGAMOTO
Wilaya ya karagwe bado inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zimekuwa kikwazo kwa hatua kubwa zaidi za maendeleo kufikiwa
Changamoto hizi ni pamoja na :-
a)     Wananchi kutokuwa tayari kuchangia miradi ya maendeleo kwa hiari hivyo kukwamisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani .
b)    Huduma za jamii hazijaweza kuwafikia wananchi kwa kiasi kinachostahili mathalani huduma ya maji afya elimu na kadhalika hivyo jitihada zaidi zinahitajika kurekebisha hali hii.
c)     Mamba za utotoni bado ni tatizo na ni changamoto kubwa inayoikabili wilaya hivyo juhudi zaidi zinafanyika kurekebisha hali hii, kama vile kuwapeleka watuhumiwa katika vyombo vya sheria na kuelimisha jamii.
d)    Uharibifu wa mazingira bado pia ni tatizo hasa uchomaji wa moto misitu hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa kurekebisha hali hii hasa kutoa onyo na elimu kwa wananchi kupitia radio za jamii zilizopo karagwe na kuchukua hatua za kisheria kwa wanaobainika kutenda vitendo vya uharibifu wa mazingira.
e)     Magendo ya kahawa kwenda nchi jirani nayo ni changamoto kwa wilaya. Hatua mbalimbali zimechukuliwa kutatua tatizo hili kubwa zaidi ikiwa ni kuweka ulinzi wa doria kwa kushirikisha uongozi na jamii katika mialo iliyobainila kuwa ndiyo vivuko haramu kuvusha kahawa.
 
4.     MATARAJIO
Matarajio ya wilaya ya karagwe katika kipindi cha miaka 50 ijayo ni kuhakikisha kuwa huduma za jamii kama vile afya elimu maji n.k. inawafikia wananchi wote wa wilaya hii.
-      kuendelea kuimalisha mawasiliano ya simu ili mitandao ya simu za mikononi iweze kiwafikia wananchi wa vijiji vyote.
-      Kuhakikisha kuwa umeme unawafikia wananchi wengi zaidi
-      Kutekeleza mipango ya kilimo ili wananchi wa wilaya hii walime kilimo chenye tija na ufugaji bora wa mifugo ya aina mbalimbali.
-      Kuinua kipato cha wilaya na cha mwananchi mmoja mmoja hasa kupitia kilimo cha mazao ya biashara, chakula na mbogamboga.
-      Kuboresha kilimo cha kahawa kama zao la biashara kwa kuwapa bei nzuri wakulima kuimalisha vyama vya ushirika sambamba na uanzishaji wa SACCOS za wakulima wa kahawa huduma za ugani kudhibiti magendo ya kahawa na kuhamasisha ununuzi binafsi ili kuleta ushindani wa bei.
-      Kuhamasisha wakulima wapande migomba ya kisasa inayostahimili magonjwa ili kuongeza uzalishaji wa ndizi kama zao la biashara na chakula.
 
Naomba kuwasilisha.

No comments:

Post a Comment