Sunday, March 17, 2013

KARAGWE WAJADILI CHANGAMOTO YA MATOKEO KIDATO CHA NNE 2012

 NA
      JUHUDI    FELIX
      KARAGWE
Serikali kuu pamoja na halmashauri ya wilaya ya karagwe , imeombwa kujali masilahi ya walimu, na kushirikiana na Wadau wa elimu  na wazazi ili kupata suluu ya kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafaunzi wanaohitimu mitihani ya kitaifa.

Hii  ni mingoni mwa maazimio yaliyotokana na   mdahalo ulioendeshwa  kwa ushirikiano wa mashirika yasiyo ya kiserikali  ya  forum syd, karadea, kademvo na MPI{Mwanza policy initative}  na wa dau wa elimu wilayani karagwe na kyerwa katika ukumbi wa kituo cha habari na mawasiliano mjini kayanga wilayani karagwe.

Awali wajumbe katika mdaharo huu wamebadilishana mawazo juu ya nini sababu zilizochangia ufaulu hafifu wa wanafunzi huku wakibainisha sababu mbali mbali zikiwemo: serikali kutojali maslahi ya waalimu, ukosefu wa nidhamu kwa wanafunzi, serikali kuingiza siasa katika elimu, kutowasilikisha waalim katika kutayarisha mitaala na sera za elimu, wazazi au jamii kwa ujumla kutowafuatilia watoto wao wakiwa shuleni na wanafunzi kutojali nini kilichowapeleka shule. 

Wakiweka maazimio ya pamoja juu ya nini kifanyike kukabiliana na hali hii, wamesema kuwa serikali kuu lazima isikilize kilio cha walimu na iache kutumia nguvu na vitisho pale wanapodai haki zao za msingi, hii ikiwa ni pamoja na  kuboresha miundombinu kama vile vitabu vilivyo na ubora, maabara, madarasa na walimu wenye sifa zinazokidhi mahitaji ili kuzalisha watalaam bora nchini.

Kwa upande wa Halmashauri ya wilaya ya Karagwe, wadau hao  wameshauri kukamilisha ujenzi wa chuo cha ualimu cha Ihanda ,kuharakisha  uanzishwaji wa kidato cha tano na sita na vyuo mbali mbali mbadala vya kuwawezesha wanafunzi kuendelea na masomo ya stadi za maisha na ufundi za kuweza kujiajiri kwa maisha yao yabadae.

Mdahalo huu  umewahusisha mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali, walimu, wazazi na wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012 zaidi ya 100 wakiwemo Mkrugenzi wa Radio fadeco,  Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha elimu wilayani Karagwe ambaye pia ni  Katibu Mkuu wa shirika la KARADEA, na wawakilishi wa wazazi.

No comments:

Post a Comment