Wednesday, December 23, 2015

PROFESA MUHONGO ASEMA VIKAO VYA BARAZA LA MADIWANI KUFANYIKA MULAGI BADALA YA MANISPAA


Mbunge  wa  Musoma  Vijijini    ambaye  pia  ni  Waziri  wa  Nishati   na  Madini  Profesa  Sospter  Muhongo  amepiga  marufuku   vikao  vyote  vya  baraza  la  madini   wa  halmashauri  ya  Musoma  Vijijini  Kufanyika  Manispaa  ya  Musoma  na    badala  yake  shughuli  zote  za  halmashauri  hiyo  zifanyike  eneo  la  Mulangi  ambako  ndiko   kunatarajiwa  kujengwa  makao  makuu  ya  wilaya.



Agizo  hilo amelitoa  kwenye  kikao cha  kujadili  mambo  ya  uchumi   na  maendeleo  ya jimbo  hilo  kilichofanyika   eneo  la  Mulangi  ambapo  amesema  kuwa  ili  kusogeza  huduma  kwa   karibu  na  wananchi  kuna  kila   sababu  vikao  na  shughuli  zote  zinazohusu   halmashauri  hiyo  kufanyika   eneo  hilo ili  ikue  haraka.

No comments:

Post a Comment