Friday, January 15, 2016

PIGO KWA CCM WAPOTEZA JIMBO HALIMA MDEE AMBWAGA WARIOBA MAHAKAMANI




Mbunge  wa  jimbo  la  Kawe  jijini  Dar  es  Salaama  kupitia  Chama  cha  demokrasia  na  Maendeleo  (CHADEMA)HALIMA  MDEE  amembwaga   mahakamani  aliyekuwa    mgombea  wa  kiti  hicho  katika  uchaguzi  mkuu  2015   kupitia  CCM    KIPPI  WARIOBA  katika  kesi  ya  kupinga  matokeo  ya  uchaguzi  huo  ambao  HALIMA  MDEE  alitangazwa  mshindi.

Mbunge  huyo  ameibuka  mshindi  baada  ya  kumwekea   WARIOBA  pingamizi  kupitia  kwa  wakili  wake Peter  Kibatara  kuwa  kesi  hiyo  ilikuwa  na  dosari za   kisheria  ikiwa  ni  pamoja  na  kutotaja  kifungu  cha  sheria  alichotumia  kufungua  kesi  hiyo.

Kutokana  na  hoja  hizo  wakili  wa  KIPPI   WARIOBA    EMMANUELI  MAKENE alikubaliana  na  pingamizi  hilo na  kuomba  kuiondoa  kesi  hiyo  mahakamani.

No comments:

Post a Comment