Na: Mbeki Mbeki
Halmashauri ya
wilaya ya karagwe Mkoani Kagera imepitisha bajeti ya shilingi zaidi billioni
49, itakayotumika katika kipindi cha mwaka 2012/2012 zitakazo tumika katika
matumizi mbalimbali ya Halmashauri hiyo.
Hayo yalisemwa jana
na kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri Ernest Mwinga Kahabi wakati akisoma makisio ya bajeti katika kikao
cha baraza la madiwani kilichofanyika kwa muda kwa siku mbili katika ukumbi wa
Angaza uliopo mjini Kayanga Wilayani humo.
Kahabi alisema kuwa
Halmashauri yake inategemea kupata jumla ya shilingi Billioni 49,184,627, 455.00 ambazo zitatumika katika
kipindi cha mwaka 2012. Hadi 2013. Katika matumizi mbalimbali ikiwemo mishahara
miradi ya maendeleo na matumizi mengineyo kwa idara zilizopata ruzuku.
Alisema kuwa kati
ya fedha hizo kiasi cha shilingi 18,052,882 ni kwa ajili ya utekelezaji wa
miradi ya maendeleo na kuwa mapato ya ndani yamekisiwa kuwa ni shilingi
3,887,446,400.00 na aliongeza kuwa kiasi
cha shilingi 27,244,776,173 kuwa ni kwa ajili ya mishahara na matumizi
mengineyo.
Aliongeza kuwa
katia ya fedha hizo kiasi cha shilingi 22,971,413,280.00 ni kwa ajili ya
watumishi na kaisi cha shilingi ni 4,273,362,893.00 ni kwa ajili ya shughuli za
uendeshaji wa ofisi.
Kahabi alisema kuwa
mapendekezo ya bajeti na mpango wa maendeleo na mwaka 2012 hadi 2013
yameandaliwa kwa kuzingatia sheria za serikali za mitaa na 7,8, na 9, za mwaka
1982 na kuwa ni kwa mujibu wa katiba ya nchi ibara ya 6,8,135 na 145.
Alieleza kuwa
mapato ya Halmashauri hiyo yatatokana na ruzuku kutoka serikalini vizuizi
vilivyo barabarani, ushuru wa mazao, mifugo na kutoka katika miradi mbalimbali
ya maendeleo.
Aidha alisema kuwa
mwongozo wa bajeti wa mwaka 2011/2012 ambao unaakisi maeneo 13 ya vipaumbele
yaliamishwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwenye uzinduzi wa Bajeti mwaka 2010
kuwa maeneo hayo ya upaumbele yanaonesha
rasilimali za umma zinakopeshwa kuelekezwa ili kuchochea maendeleo na
kushughulika matatizo ya nchi jamii na kiuchumi.
Hata hivyo baraza
la madiwani wa Halamashauri hiyo
waliipitisha Bajeti hiyo na kushauri kuwa Bajeti hiyo itumike kwa makusudio
yaliyo kusudiwa na kuonyesha matumizi
mabaya ya fedha za umma zinazotumika kwa manufaa ya wachache kuwa hawatavumilia
watumishi wa aina hiyo.
No comments:
Post a Comment