Na: Mbeki Mbeki
Baraza la madiwani
la Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe limekataa kupitisha mradi wa kitega uchumi
chenye thamani ya shilingi billion 50, kutokana na kuhusishwa na vitendo vya rushwa.
Chanzo cha habari
hizi kimeeleza kuwa madiwani wote bila kujali itikadi zao za vyama wameukataa
mradi huo, ambao wamedai umeghubikwa na harufu ya ufisadi ambapo walieleza kuwa
kitega uchumi hicho kilikuwa kijengwe
kwa kukopwa na benki ya ADB kwa
kushirikiana na NSSF.
Madiwani hao ambao
hawakuwa tayari kutaja majina yao katika vyombo vya habari walisema kuwa baada
ya kikao cha kawaida cha baraza la
madiwani walikaa kama kamati kujadili ujenzi wa kutega uchumi ambacho walisema
awali kilikuwa kimekadiriwa kugharimu jumla ya
shilingi Billioni 27,600,000/= kiasi ambacho kitatolewa na NSSF kama mkopo kwa halmashauri za
Kyerwa na Karagwe.
Chanzo cha habari
hizi kilieleza kuwa madiwani hao waliamua kukataa kutokana na kwamba agenda
hiyo ililetwa na mwenyekiti wa Halmashauri hiyo bila kufuata maazimio ya vikao
na kuwa alishindwa kulieleza baraza lake ni kwa namna gani wataweza kulipa deni
watakalo kuwa wamekopwa na kuwa ni nani atakayesimamia mradi huo katika hatua
nyingine madiwa hao walieleza kuwa eneo lililokusudiwa kujenga kitega uchumi ni
eneo lililokusudiwa kujenga kwa ajili ya stendi ya magari kuwa mchakato mzima
wa ujenzi ulipaswa kuwashirkisha wananchi
ambao ndio wadau wa kubwa wa Halmashauri na maendeleo kwa ujumla.
Pia chanzo cha
habari hizi kilieleza kuwa eneo hilo lilishagawiwa kwa wananchi ambao walitaka
kujenga vyumba vya kukodisha kwa ajili ya kuzunguka stendi ya magari, amabpo
walisema nao walipaswa kushirikishwa, jambo ambalo walisema halikufanyika.
“ Ninachoweza
kukueleza bila uficho ni kwamba mwenyekiti wetu anataka kutuburuza kwa maslahi
yake ukisoma kwenye kablasha letu uk.19 yaliyoandikwa ni uongo madiwani
hatujakubaliana na mtu katika uejnzi wa kitega uchumi” Alisema.
Uchunguzi
ulionyesha kuwa hata kamati ya fedha ya Halmashauri ilikataa shinikizo la
mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kutaka ujenzi huo uanze mara moja na kuwa baraza
la madiwani lipitisha kiasi cha milioni 15 kwa ajili ya kuanza mchakato wa ujenzi.
Aidha madiwani hao
walikataa kuwahi kufanya makubaliano ya
kkujenga kitega uchumi cha stendi katika mji wa kayanga uliopo wilayani hapa na
kuingia makubaliano na mashauri msanifu wa majengo wa kampuni ya CONS AFRICA LIMITED na kufadhiliwa na
shirika la hifadhi ya jamii (NSSF). Hata
hivyo madiwani hao walisema kuwa yapo makampuni na watu binafsi wanaoweza
kuwajengea mradi kama huo wenye gharama zinazokopesheka kulingana na mapato ya
Halmashauri yao.
“ Huyu mwenyekiti
anataka tushindwe kufanya kazi za maendeleo na tufikirie kulipa madeni, na hili litatupelekea kupiga kura ya kutokuwa
na imani naye kwani theruthi mbili zikimkataa tunastisha uchaguzi tumechoka
kuburuzwa” Alisema.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa Halmashauri hiyo
kushunju runyogoote alipohojiwa kuhusiana na tuhuma zilizoelekezwa kwake
alisema kuwa ameshindwa kuelewa kwanini madiwani wenzake wameamua kumgeuka na
kupigana na maazimio waliyowahi kuyaazimia.
Runyogote
alikanusha kuwa hakuna miaya ya nushwa inayoenelekezwa katika ujenzi wa mradi
huo bali ni suala zima la kuwatetea wananchi maendeleo.
Aidha uchunguzi wa
haabri hizi umeonyesha kuwa kikao cha dharula
cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo kimeitishwa tena mei 23 mwaka
huu katika hali ambayo imeelezwa kuwa ni katika mstakhabali wakunusuru kati cha
mwenyekiti au kura ya kutokuwa na imani na nafasi akiyo nayo.
No comments:
Post a Comment