Friday, August 3, 2012

DREVA NAO NGARA WACHACHAMAA KULIKONI?

Madereva wa vyombo vya usafiri wilayani Ngara  wataka mikataba ya kazi toka kwa waajiri wao
 
 
Madereva wa vyombo vya usafiri walioko wilaya ya Ngara mkoani Kagera wamewataka wamiliki wa vyombo hivyo kuwapa mikataba ya kazi ikiwemo mishahara  kwa mwezi  pamoja na kupunguza kiwango cha mawasilisho ya fedha kwa siku ili wafanye kazi zao kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani
 
Mmoja wa Madereva mjini Ngara Medard Mpanju alitoa kauli hiyo Julai 28 katika kikao cha wamiliki wa vyombo vya usafiri , madereva na kikosi cha usalama barabarani kilichoongozwa na mkuu wa Wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyasu kwenye ukumbi wa Paradise mjini Ngara
 
 Mpanju alisema kuwa maderva wanafanya kazi katika mazingira magumu kwa kulazimika kubeba abiria wengi katika chombo cha usafiri ili kuwasilisha mapato kwa tajiri kati ya shilingi elfu 30 hadi elfu 40 kwa siku na hatimaye kujikuta wakivunja sheria kwa kubeba abiria kupita kiasi ukiwemo mwendo kasi katika vituo vyote wilayani humo
 
 Wakati huo huo madreva wa pikipiki wanaofanya kazi ya kubeba abiria katika wilaya hiyo  walisema wanafanya kazi katika
mazingira magumu kutokana na changamoto ya kukosa leseni kutoka makao makuu ya wanafanya kazi katika mazingira magumu kutokana na changamoto ya kukosa leseni kutoka makao makuu ya mkoa ambapo  kazi yao inakuwa ngumu kwa kukimbizana na jeshi lapolisi  hasa askari wa usalama barabarani kwa kuwa hufanya kazi kwa kuvunja sheria na kusababisha kuwepo mianya ya rushwa kwa askari wasio waadilifu kwenye kazi yao
 
Mwenyekiti wa madereva hao Yazzidu Wilsoni  Masha   alisema kwa sasa wamejiunga katika vikundi vya kukopeshana kupata mafunzo na leseni lakini kero kubwa ni kupata leseni toka makao makuu ya mkoa ambapo ni mbali na wilaya hiyo  wanakofanyia kazi zao za kusafirisha abiria
 
“Tumeanza  kuunda umoja wa  kuchangiana kupata leseni  kwa kila mmoja kuchangia shilingi  elfu 60 kila mwezi  na kulipia shilingi  elfu tano kila siku ili baadaye  kupata shilingi milioni mbili ili kuwa na chombo binafsi kwa lengo la kujiajiri” AlisemaWilson Masha
 
Alisema pia serikali kupitia tanroard iweke ishara za alama za usalama barabarani na halmashauri wilayani humo kuweka miundombinu rafiki kwenye standi za magari katika vituo vya Ngara mjini ,Kabanga ,Rulenge na Benaco kwa kuwa magari yanayoingia katika vituo hivyo hulipia ushuru kama vyanzo vya mapato
 
Hata hivyo mkuu wa jeshi la  polisi wilayani Ngara Mohamed Milanzi alisema jeshi la polisi wilayani humo litahakikisha sheria zinafuatwa na kuondoa changamoto zilizopo kwa wamiliki wa magari  pikipiki wakiwemo madereva  wa vyombo hivyo likiweo na jeshi lenyewe .
 
Milanzi aliwataka askari wa usalama barabarani wanaokiuka maadili ya kazi zao kuhakikisha wanatambua miiko ya kazi kwa kuepuka rushwa uonevu na vitisho au kujichukulia sheria mkononi na kuhatarisha usalama kwa raia na mali zao jambo la msingi ni kuhamasisha jamii kutii sheria bila kushurutishwa.
 
Katika hatua nyingine Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyansu aliwataka wamilikina waendesha vyombo vya usafiri kufanya kazi kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali zisizo za lazima na kuendelea kuhatarisha maisha ya watu huku serikali ikipoteza watu ambao ndio wanaotegemewa katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya Taifa
 
Kanyasu  alisema ili chombo kiweze kufanya kazi barabarani  ni bora kisiwe na hitilafu, sambamba na kufuata taratibu za kupakia abiria na mizigo ili kuhakikisha chombo kinakuwa katika hali ya usalama  pamoja na abiria huku wakiepuka mwendo kasi ambao hushindwa kusoma hata alama za Tan Roard zilizopo kwenye maeneo wanakopita .
 
Aidha alitoa muda wa miezi miwili kwa maderva wa vyombo vya usafiri wasio na leseni kuhakikisha wanazitafuta na kuzisajili ili kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na  jeshi la polisi lifanye utaratibu wa kuwahamasisha watoa leseni mkoani kufika wilayani Ngara kuwakatia  leseni hizo pamoja na mafunzo  ya sheria  ili kurahisisha kazi zao.
 
Mkutano huo ulifanyika baada ya kuwepo migogoro kari ya madereva na jeshi la polisi miezi miwili iliyopita ambapo askari mmoja alimpiga dereva kwa kukiuka sheria ya kujaza abiria wengi na kumsababishia maumivu na kulazwa katika Hospitali ya Nyamiaga wilayani humo na askari waliohusika kesi yao inasikilizwa katika mahakama ya kijeshi mkoani Kagera
 
Ikiwa ni hatua ya kutafuta ufumbuzi wamatukio ya ajali za barabarani zinazo tokea mara kwa mara wilayani Ngara mkutano huo ulihusisha pande zote mbili serikali na vyombo vyake vya dola vinavyosimamia sheria na wamiliki wa vyombo vya usafiri pamoja na watumiaji wa kila siku wa vyombo hivyo ambavyo huingia barabarani huku vikiwa na lengo la kumsaidia mjasilia mali kupambana na umaskini hapa nchini.
   
 
 

No comments:

Post a Comment