Tuesday, January 22, 2013

WATUMISHI WAASWA KUJITUMA


 NA
      JUHUDI  FELIX
KARAGWE

Watendaji wa halmashauri nchini wametakiwa kusimamia vema miradi ya maendeleo na kuwa na uadilifu na uwajibikaji kwa serikali iliyopo madarakani kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wake.

Agizo hilo limetolewa na  mkuu wa Mkoa wa Kagera  Kanali Mstaafu Fabian Massawe katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye   wilaya ya Karagwe wakati akiongea na viongozi na watendaji wa halmashauri hiyo.
Amesema kuwa endapo viongozi watasimamia vema  miradi ya maendeleo na kuongoza wananchi  kwa uadilifu  ufanisi katika shughuli za maendeleo utakuwepo  na seikali iliyopo madarakani  itatimiza malengo yake  ya kuwahudumia wananchi wa kada zote na kuondoa manunguniko yaliyopo kwa sasa.

Aidha,Kanali Massawe ametoa agizo  kwa wazazi na walezi  kuwapeleka  watoto wao waliochaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari  ndani ya wiki moja ,kauli hii ameitoa baada ya mkuu wa shule ya sekondari ya Ndama kusoma taarifa iliyobainisha  mapungufu   wanafunzi 200 waliochaguliwa kujiunga na shule hiyo kati yao waliripoti na kuanza masomo ni wanafunzi 40 tu.

Katika ziara hiyo mkuu wa Mkoa ameweza kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo  mradi wa ujenzi wa chuo cha ualimu  Karagwe kilichopo kata ya Ihanda,mradi wa umwagiliaji wa Mwisa Bujuruga,mradi wa maji wa Charuhanga,Shule ya sekondari ya Kiruruma kukagua ujenzi wa bweni la wasichana,kutembelea Zahanati ya Omurusimbi kwa ajili ya kukagua ukamilishaji wa ujenzi wake na kutembelea shirika la Mavuno kukagua miradi mbalimbali ya shirika hilo.
  

No comments:

Post a Comment