NA
JUHUDI FELIX
KARAGWE
Wazazi na walezi wametakiwa kutoa fursa sawa kwa watoto wao wa kike na
wakiume ili kuwepo uwiana ulio sahihi katika kupata elimu na kuleta ushindani
kwa jinsia zote bila ya upendeleo.
Wito huo umetolewa na Afisa elimu wa wilaya wa shule za sekondari Hellen Rugumira wakati akihutubia maafali ya kumi na
tatu ya kidato cha sita katika shule ya
Karagwe sekondari. Amesema kuwa mara nyingi wazazi na walezi wanatoa fursa kwa
watoto wa kiume kupumzika na kupata muda mwingi wa kupumzika na kujisomea huku
watoto wa kike wakikosa muda wa kujisomea kwani ndio wanakuwa wasaidizi wa shughuli za nyumbani warudipo nyumbani.
Rugumira pia amewataka wanafunzi kutumia vikao vyao
halali vya shule kujadili na kuwasilisha changamoto zinazowakabili kwa uongozi
na kuwataka wanafunzi kuongeza bidii katika masomo na kazi nyingine zo za
kujitegemea.Pia ametoa zawadi kwa shule
hiyo ili kuongeza kasi ya ufaulu zawadi hiyo ya miongozo ya kufundishia kwa
walimu.
Mwenyekiti wa
bodi wa shule hiyo Askofu mstaafu wa Diyosisi ya Karagwe Nelson Kazoba akitoa nasaha zake kwa wazazi
,wanafunzi na wageni waalikwa amesema
kuwa kuna uvumi usiokuwa na ukweli ndani yake unaoenezwa mitaani na baadhi ya watu
wasiipendea mema shule hiyo kuwa imeshuka
kitaaluma au haipokei wanafunzi na kuwatakuwa wasichafue shule hiyo na
kuwataka watu na jamii kwa ujumla kupata
taarifa kwa vyanzo sahihi vya uongozi wa shule hiyo.
Naye kaimu mkuu
wa shule hiyo Donasian Rufulano akitoa neon la kuwaaga wahitimu hao
amesema kuwa waendeleze malezi bora na ujuzi waliopata katika shule hiyo na
wawe mfano bora kwa jamii. Ameongeza kuwa tayari kuna chuo kutoka nchini Costarica kimetoa
nafasi kwa wahitimu kujiunga nacho baada ya taratibu zote za usajili kukamilika
na kuongeza kuwa fomu hizo zinapatikana katika ofisi ya taaluma shuleni hapo.
Kwa upande wao wahitimu wakisoma risala kwa mgeni rasmi wamesemakuwa wanapongeza uongozi wa shule kutatua tatizo
la uhaba wa walimu haswa wa sayansi mbali na kupainisha pongezi hizo wameuomba uongozi wa shule hiyo kuitisha
mikutano ya wazazi ,kutumia lugha ya kiingereza kwa shughuli zote za
shule hata wakaomba pia iandaliwe sara kwa lugha hiyo ili waweze kuimudu na
kuleta ufaulu kwa masomo yao.

No comments:
Post a Comment