Thursday, December 24, 2015

MWILI WA ASKARI PETER SIMON ALIYEPIGWA RISASI NA MWENZAKE JANA WAAGWA RASMI JIJINI MWANZA.


Jeneza  la  Polisi   Petro   Simon   aliyepigwa  risasi  na  askari  mwenzie, likiwa eneo  la  polisi  Mabatini  Mwanza   wakati  wa  ibada  ya  kuaga  mwili  wa   Marehemu.

Askari  wawili   wa  jeshi  la  polisi  jijini  Mwanza  wamefariki   dunia  baada  ya  mmoja  kumuua kwa  kumpiga  risasi  mwenzake   kabla  na  yeye  kujimaliza  kwa  kujipiga   risasi  tukio  hilo  lilitokea  jana   alasiri  eneo  la  benki  ya Posta   barabara  ya  Pamba   jijini  Mwanza.





Waombolezaji  wakitoa  heshima  zao  za  mwisho.



Kamanda  wa  Polisi  mkoa  wa  Mwanza  Justus  Kamugisha   alithibitisha  kutokea  kwa  tukio  hilo   na  kusema  tayari  jeshi  hilo    limeanza  uchunguzi  kubaini   chanzo  cha  mauaji  hayo.


No comments:

Post a Comment