Sunday, March 17, 2013

CHANGAMOTO ZIKIWEKWA WAZI KUTATULIWA NI LAZIMA



Na
    JUHUDI  FELIX
     KARAGWE.
Watu wenye ulemavu wametakiwa kujiunga na vikundi mbalimbali vya kuweka na kukopa ili kujikwamu na hali duni ya kiuchumi,kuondoa tabia ya kulalamika na omba omba.

Wito huo ulitolewa na Mkuu wa wilaya ya Karagwe Bi Dary  Ibrahimu  Rwegasira wakati akitoa hotuba yake ya ufunguzi kwenye mdahalo wa kujadili changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu ulioandaliwa na uongozi wa Chama cha watu wenye ulemavu wa viungo Chawata mkoa kwa ufadhili wa The Faoundation for civil Society.

Alisema kuwa watu wenye ulemavu wakijiunga kwenye vikundi vya kuweka na kukuopa yaani vikoba itakuwa ni mkombozi kwao ili kuondokana na hali ya kuomba omba na kulalamika huku wakiboresha maisha yao.

Bi  Rwegasira alisema kuwa watu wenye ulemavu wakiwa kwenye vikundi ni rahisi kuwasaidia na kujiunga na huduma mbalimbali za kuwasaidia kupunguza makali ya maisha na ametolea mfano wa huduma ya Bima ya Afya wakijiunga kwa kuchangia wataweza kutibiwa kwa gharama nafuu kuliko kulipia kupitia mfumo wa kawaida.

Awali Laurian Pankrasi  akisoma risala kwa mgeni rasmi mwenyekiti wa Chawata mkoa pia katika mradi huu anajulikana kama mratibu amesema kuwa lengo la mdahalo ni kujadili sera ya maendeleo ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004 na sheria ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2010 kwa ajili ya kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu kujua haki zao za msingi.

Wakichangia mada hiyo wajumbe mbalimbali waliohudhuria mdahalo huo wamebainisha changamoto mbalimbali zikiwemo kutoshirikishwa katika nyanja za maamuzi,kupata fursa sawa ya katika Elimu,ajira, huduma ya Afya,usafiri na kutokuwepo miundo mbinu ambayo si rafiki kwa watu wenye ulemavu kwenye majengo ya umma.

Changamoto nyingine ni kujinyanyapaa watu wenye ulemavu wenyewe na kutokuwa na lugha ya usawishi wa kuwasilisha hoja zao kwa watoa huduma na kuishia kulalamika bila kuweka bidii ya kuwa waadilifu na urafiki  na wanajamii.

Mdahalo huo ambao ulihudhuliwa na watu wenye ulemavu,viongozi wa taasisi za dini,Viongozi wa Vyama vya siasa,Wanasheria ,madiwani na wataalamu kutoka idara za serikali za ustawi wa jamii,maendeleo ya jamii,Mipango  na idara nyinginezo.






No comments:

Post a Comment