Sunday, March 17, 2013

JITIHADA ZA MAKUSUDI ZAHITAJIKA



 NA
      JUHUDI  FELIX

KARAGWE

Mamlaka ya maji safi na taka  mjini Karagwe  KAUWASA  inakabiliwa na changamoto  mbalimbali  ikiwemo uhaba  wa vyanzo vya maji vyenye uwezo wa  kuhudumia  idadi kubwa ya watu wanaoongezeka kwa kasi  katika eneo la mjini  na vitongoji vyake.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya karagwe  Bosco Ndunguru  hivi karibuni  kwenye kikao cha baraza la madiwani  kilichofanyika kwenye ukumbi  wa vijana Angaza mjini kayanga.

Amesema mamlaka ya maji  mjini inakabiliwa na changamoto  mbalimbali  ikiwemo uwaba wa vyanzo vya  maji  vyenye uwezo wa keweza kuhudumia  idadi  kubwa ya watu  wanaoongezeka  kwa kasi katika eneo la mjini  na vitongoji vyake  jirani.


Changamoto nyingine ni ufinyu wa fedha za kuendeleza  na kuweza kuwa na vyanzo vya maji vyenye uwezo wa kuzalisha  maji ya kutosheleza mahitaji ya mjini,garama kubwa za uendeshaji  kwa upande wa vipuli  vya mitambo  na vile vya miundombinu  ya mabomba  ,ubora wa maji usiokidhi viwango vinavyotakiwa  kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha wa kujenga mitambo ya kutibu maji nan fedha za inunuzi wa madawa.


Amesema kuwa.kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013  mamalka ya maji ilikadiria  kukusanya kupitia vyanzo vyake  vya ndani  jumla ya shiling milioni sitini na mbili mia tano tisini na tisa elfu  mia tatu sitini na nane na senti ishirini na tano ambapo amesema hadi January 2013  ilikuwa imekusanya jumla ya shilingi milioni mia nane na thelathini tano  mia tisa thelathini elfu  mia saba  sabini na tatu  sawa na asilimia 53 .4 ya lengo la mwaka.

Aidha amesema ofsi yake imeandaa mpango wa ukarabati  wa mradi wa maji kwa chanzo cha charuhanga  kwa manufaa ya kutoa huduma  ya maji  kwa wakazi wa mij wa Omrushaka  na vijiji vyake jirani.

Hata hivyo amesema kuwa  kuna mambo kadhaa  ambayo yamefanikishwa na ofsi  ya mkurugenzi mtendaji  ikiwa ni pamoja na kununuliwa  kwa mtambo mpya  wa kusukuma maji SP 8A YS  kwa chanzo cha maji  cha wateja wapya 29 .kuunganisha huduma ya maji  na kufanya jumla ya wateja  413 hadi janualy mwaka huu.

No comments:

Post a Comment