Wednesday, December 23, 2015

AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA BAADA YA KUKUTWA NA HATIA YA KULAWITI MTOTO.


Mahakama  ya  wilaya  ya Ilala imemuhukumu  kifungo  cha   cha  Maisha   Seleman Nassibu  mwenye  umri  wa  miaka  (20) baada  ya  kupatikana  na  hatia  ya  kumlawiti   mtoto  wa  kiume  mwenye   umri  wa  miaka  13.

Nassibu  ambaye  ni  mkazi  wa  Majohe   amehukumiwa  kifungo  hicho  baada  ya  mahakama  kujiridhisha  na  ushahidi  wa  mashahidi wanne  uliotolewa   mahakamani  hapo.

Akisoma  hukumu  hiyo   Hakimu  Mkazi   Mfawidhi  wa  mahakama  hiyo   Said  Mkasiwa  amesema  mahakama  imemtia   hatiani   baada  ya  mashitaka  kudhibitisha   mashtaka  hayo  bila  kuacha  shaka.

Kabla  ya  kutoa  adhabu hiyo  wakili  wa  serikali  Eric  Shija  aliiomba  mahakama   kutoa  adhabu  kali  kwa  mshitakiwa  ili  iwe  fundisho  kwa  wengine.

No comments:

Post a Comment