Wednesday, December 23, 2015

MFANYABIASHARA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 20 JELA YA KUTIWA HATIANI KUHARIBU MIUNDOMBINU YA RELI.


Mfanyabiashara   Andrew    Gatawa  amehukumiwa  kifungo   cha  miaka  20  jela   baada  ya   kupatikana  na   hatia  ya   kuharibu  miundo mbinu  ya  reli.

Gatawa  amehukumiwa   kifungo  hicho   katika  mahakama  ya   Ilala   baada  ya  kupatikana   na  hatia  ya  kung’oa   mataruma   ya  reli  ambayo  ni  mali  ya  Mamlaka  ya   Reli  Tanzania   na  Zambia  (TAZARA)

Mahakama  imewaachia  huru  washitakiwa  wawili  ambao walikuwemo  katika    kesi  hiyo  kutokana  na   upande  wa  mashitaka   kushindwa  kuthibitisha   mashtaka  dhidi  yao   hivyo  kushindwa  kuwatia  hatiani .

Akisoma  hukumu  hiyo   Hakimu   Mkazi  wa  Mahakama    hiyo  Flora   Mujaya  amewataja   washtakiwa   walioachiwa  huru   na  mahakama   kuwa  ni  Issa  Seif  na  Abdallah  Hamidu   kutokana  na   upande  wa  mashitaka   kushindwa  kuthibitisha   mashitaka  hivyo  kushindwa  kuwatia  hatiani.

No comments:

Post a Comment