Wananchi
wa Kijiji cha
Nyabwegira wametoa wito
kwa uongozi wa
halmashauri ya wilaya
ya Karagwe kuhakikisha
wanatafuta haraka ufumbuzi
wa tatizo la
kutokuwa na mwenyekiti
wa serikali ya
kijiji hicho kwani
unasababisha shughuli nyingi
za maendeleo zinakwama
kwa kukosa uongozi
huo.
Wametoa wito huo jana wakiwa katika shughuli za kujitolea kwenye chanzo cha maji Kifunjo kilicho kwenye kitongoji cha Kilifunjo B na A ambao waliungana kufanya usafi wa chanzo hicho wakiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Edward Mpaka wananchi hao walisema kutokuwa na mwenyekiti wa serikali ya kijiji kunasababisha shughuli nyingi za maendeleo kukwama na kudhoofisha jitihada zao
Peter
Martine alisema kutokuwa na
mwenyekiti ni chanzo
cha matatizo ya
shughuli za maendeleo
kukwama na kumtaka
Afisa Mtendaji wa
kata hiyo David
Itegereize kulitolea majibu
kwani aliwahaidi wananchi wa
kijiji hicho kulitafutia
ufumbuzi tatizo hilo
ndani ya muda
wa mwezi mmoja
lakini hajawahi kuwapa
mrejesho.
Naye
Hamdani Hamada mkazi
wa kitongoji cha
Kilifunjo A amesema
kuwa tatizo hilo
ni liinakwamisha shughuli
nyingi huku likitawaliwa
na itikadi za
siasa miongoni mwao
huku akimtaka Afisa
Mtendaji kulitolea kauli
na ambao wataendelea
kufanya hivyo hatua
zichukuliwe.
Diwani
wa Kata ya
Ndama Edward Mpaka
amesema anawapongeza wanbanchi
wa vitongoji viwili
vya Kilifunjoa A
na Kilifunjo B
kujitokeza kwa wingi
kufanya shughuli za
maendeleo kwa kujitolea
na kuwata kuendelea
na moyo huo
wa kupenda maendeleo
na kufanya hivyo
kata hiyo itasonga
mbele.
Akizungumzia
suala la kijiji hicho
kutokuwa na mwenyekiti
amesema wanamtaka mkurugenzi
kuitisha uchaguzi kwa
mujibu wa sheria
inavyoeleza kwani mwenyekiti
aliyekuwepo hukumu ilishatolewa
na hakukata rufaa
hivyo hatakiwi kuendelea kumiliki nyaraka
za serikali na
inabidi azikabidhi mara
moja.
“Tunamtaka
mkurugenzi mtendaji wa
halmashauri ya Karagwe
wala hamtumuombi maana
sheria inasema hivyo
aitishe uchaguzi ndani
ya siku 60 sasa
tunamiezi nane tangu hukumu
itolewe na aliyekuwa
mwenyekiti hakukata rufaa
yoyote hivyo nakuagiza
mtendaji mtu anayemiliki nyaraka
hizo awe ameziwasilisha kwako
kabla ya Januari 05
mwakani “Alisema Mpaka
Aliyekuwa
mwenyekiti wa Kijiji
cha Nyabwegera Sadick
Athumani ambaye katika
uchaguzi wa serikali
za mitaa alikua
amepita bila kupingwa
baada ya kumwekea
pingamizi mshindani wake
lakini CHADEMA walifungua
kesi mahakamani na
hukumu ilitolewa na
ushindi huo ulitenguliwa
na mahakama ya
wilaya ya Karagwe.
Kwa
upande wake afisa
Mtendaji wa Kata
ya Ndama David
Itegereize amesema kuwa suala
hilo la mwenyekiti
wa kijiji ameishaliwasilisha kwenye
ngazi husika ili
ziweze kulifanyia kazi
hivyo pindi atapopewa
majibu atayawasilisha kwao
mara moja.
Aliwataka
watu wote wanaofanya
shughuli za kibinadamu
kwenye vyanzo vya
maji kwenye kata
hiyo kuhakikisha anasitisha
shughuli hizo mara
moja vinginevyo utaratibu
wa sheria zitatumika
maana mtu haruhusiwi
kufanya shughuli yoyote
ndani ya mita
60 kutoka kwenye
chanzo cha maji.
No comments:
Post a Comment