Sunday, January 3, 2016

VIJANA KARAGWE WAANZA MWAKA NA MILIONI 48 ZA SERIKALI TOKA WIZARANI WAJIPANGA KUPEANA MIKOPO.





Chama  cha  ushirika  wa  kuweka  na  kukopa   cha  Karagwe  Vijana  Saccoss(KAVISA)  kimepata  mafanikio  mbalimbali  tangu  kuanzishwa  kwake  mwaka  2013  ikiwemo  kuongeza  wanachama  pamoja  na  kutoa  mikopo  kwa  vijana  iliyosaidia    kujikwamua  kimaisha  na  kujiajiri  na  kuondokana  na  ukosefu.







Akisoma  taarifa  ya  bondi  ya  chama  hicho  mwenyekiti  wa  ushirika  huo  ujulikano  kwa  ufupi   KAVISA    David  Geofrey  amesema  kuwa  wanachama  wameongezeka  tangu  kuanzishwa  kwake  pia  akafafanua  kuwa   ushirika  huo  haufungamani  na  upande  wowote  wa  itikadi  za  udini,siasa  wala  ubaguzi  wowote  ule.

Amesema  kuwa  KAVISA  imefanikiwa  kuwaunganisha  vijana  na  wameweza  kutoa  mikopo  kwa  ambayo  imekuwa chachu  ya  kuanzisha  miradi  mbalimbali  ya  kujiajiri  huku  akibainisha  mafanikio  kadhaa  ambayo  ni  pamoja  na  kuongeza  wanachama  wa  ushirika  huo.

Geofrey  amebainisha  changamoto  zinazokabili  KAVISA  kuwa  ni  kutokuwa  na  viongozi  haswa  nafasi  ya  katibu  na  mhasibu  na  walioajiriwa  walishiriki  kukiingiza  chama  kwenye  hasara  kubwa   kama  ambavyo  hapa  amabainisha.






Afisa  maendeleo  ya  Jamii  wilaya  ya  Karagwe  Edina  Kabyazi  ambaye  amekuwa  mlezi  wa  KAVISA  SACOSS  amesema  anatamani  kuona  ushirika  huo  ukikua  na  kuwa  mkubwa  na  kusema  kuwa   ataendelea  kutoa  ushirikiano  kama  ilivyokuwa  mwanzo  na  kueleza  kuwa  sasa  wamempata  Afisa  Maendeleo  ya  Vijana  wamtumie  kwa  karibu  kwani  ndiye  mhusika  zaidi.
.
Hata  hivyo  wajumbe  wa  mkutano  mkuu  wa  Karagwe  vijana  SACOSS  wamempongeza  mwenyekiti  kwa  kuendelea  kuongoza  chama  hicho  licha  ya  kuwa  na  mazingira  magumu  ya  kuendesha   ofisi  mkutano  huo  pia  umehudhuriwa  na  afisa  ushirika  Jones  Rweyunge  ambaye  naye  amekuwa  msaada  mkubwa  kwa  vijana  hao.

No comments:

Post a Comment