Jumla ya shilingi Billioni
500 zinahitajika kukamilisha ujenzi
shule ya watoto walemavu walipo katika
halmashauri ya wilaya ya karagwe mkoani kagera.
Kauli hiyo ilitolewa jana na
sisita Godeliva Mboyerwa kutoka jimbo la
kikatoriki ka kayanga katika semina iliyowahusisha walemavu 42, iliyofanyika katika ukumbi wa
Angaza wa halmashauri hiyo iliyopo mjini Kayanga.
Sista mboyerwa alisema kuwa
jumla ya shilingi billioni 500
zinahitajika kukamilisha ujenzi wa shule ya msingi mwoteka center inayoendelea
kujengwa kata ya Nyabiyonza, kijiji cha Chabalisa na kanisa katoriki kwa
kushirikiana na Halmashauri ya wialya ya karagwe.
Alisema kuwa shule hiyo ya
walemavu inajengwa kwa madhumuni ya kukuza na kuimalisha vipaji vyao
kuwapunguzia mazingira hatarishi, kuwapa
upendo katika kuwahudumia kuwa ni pamoja
na kuwafanya kuwa sawa na watoto wengine wasio na ulemavu katika
mahitaji ya kielimu, ambapo aliongezea kuwa madarasa mawili yameisha kamilika na kuwa shule hiyo
itakuwa ya bweni ambayo haitakuwa na itikadi yadini yoyote.
Sista Mboyerwa alisema kuwa
wanacnhi waondokane na dhana potofu ya
kuwanyanyapaa walemavu na kuwa walemavu wanayo haki sawa na watu wengine kuwa
wananchi wanapaswa kuchangia ujenzi wa shule hiyo inayoendelea kuejngwa. Kwa upande wake
mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya
hiyo Kashunju Runyogote alisema kuwa katika ujenzi wa madarasa
Halmashauri imechangia shilingi milioni 25, ujenzi wa bweni shilingi milioni
74, na kuongezea kuwa katika mwaka wa fedha 2012 hadi 2013, zimetenhwa shilingi
milioni 120 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa shule ya walemavu.
Aidha alisema kuwa
halmashauri hiyo imetenga shilingi milioni 95. Kwa ajili ya kuwalipia wanafunzi
wenye ulemavu wa ngazi karo wanasoma
katika shule ya walemavu iliyopo
Kitengure Mkoani Kagera.
Hata hivyo, amewataka
viongozi wa vijiji na kata kuwaorodhesha watoto wote wenye ulemavu wa aina
yoyote ili shule itakapofunguliwa waweze kusajiliwa na kuanza masomo na
kuongezea kuwa walimu watakaofundisha katika shule hiyo watakuwa ni wenye elimu
maalum na kuwa Halmashauri hiyo kwa kushirikiana na Kanisa wanakusudia kuifanya shule ya mchepuo wa kiingereza.
No comments:
Post a Comment