Wednesday, June 6, 2012

CHANZO CHA KUSHUKA ELIMU KARAGWE SABABU HIZI HAPA



Na Mbeki Mbeki

Imebainika kuwa chazo cha ufaulu hafifu kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika wilaya ya karagwe kinasababishwa na walimu wengi kukaa mbali na vituo vyao vya kazi.

Kauli hiyo iliyotolewa jana na baadhi ya wadau wa elimu  wilayani hapa kuwa wamebaini kuwa asilimia kubwa ya walimu wanakaa mbali na vituo vyao vya kazi hivyo kushindwa kufundisha vipindi vyote vya masomo kwa muda unaotakiwa.

Walisema kuwa hali hiyo imesababisha walimu hayo kuchelewa kuripoti shuleni na kuwahi kuondoka  kabla ya muda wa kazi hivyo kushindwa kufundisha baadhi ya vipindi.

Waliongeza kuwa tatizo hilo limesababisha wanafunzi wengi kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yao na baadhi yao kuhitimu bila kujua kusoma na kuandika ambapo wanafunzi 59 katika shule mbalimbali za sekondari wilayani hapa wamebainika hawajui kusoma kuhesabu na kuandika.

Mmoja wa wadau hao, Anthon Cleophace alisema kuwa kushuka kwa kiwango cha elimu katika wilaya yao kunachangiwa na kutokuwa na mwamko wa kuchangia shughuli mbalimbali za elimu.

Alisema kuwa shule nyingi zilizopo pembeni mwa Halmashauri hiyo kuwa zinahuaba wa nyumba za walimu hali inayochangia uzorotaji wa ufundishaji kutokana na kuwa na wanafunzi wengi tofauti na idadi ya walimu waliopo.

Aidha alisema kuwa tabia ya walimu wengi katika wilaya hiyo kujihusisha na suala la mikopo kumechangia kushusha taaluma katika mashule yao, kuwa walimu wanashinda mijini kushughulikia mikopo na kutafuta makampuni yanayokopesha na kuwaacha wanafunzi bila huduma yoyote mashuleni.

No comments:

Post a Comment