Wednesday, June 6, 2012

WANAKAGERA WAASWA KUEPUKA MATENDO MAOVU

Na Mbeki Mbeki

Wananchi mkoani kagera wametakiwa kutojihusisha na vitendo viovu vinavyochangia kuvuruga amani ndani ya jamii ili weweze kuimalisha utawala bora nchini

Mkuu wa mkoa wa kagera kanali msitaafu Massawe ameyasema hayo wakati akifungua mkutano mkuu kati ya wadau wa utawala bora wa mkoa wa kagera timu ya tathimini ya utawala bora wa Afrika (APRM) katika hotuba iliyo……….. na katibu tawala wa mkoa wa kagera, Nassoro Mnambila.

Alisema vitendo vya mauaji ya vikongwe na albino ambayo yanaenda sambamba na imani za ushirikina na tohara wanazofanyiwa wanawake vinachangia kuangusha sifa mabayo Tanzania inayo ya kuzingatia masuala ya utawala bora.

Alisema kuwa Tanzania inazingatia na itahakikisha inaendelea kuzingatia utawala bora ambapo alisema utawala bora nchini inawapa wananchi nafasi kubwa ya kujadili mambo yanayowagusa viongozi.

Aidha kanali mstaafu Massawe aliwaomba washiriki wa kikao hicho kuwakilisha hoja sahihi zinazohusiana na masuala ya utawala nchi ili kamati ya tathimini iliyoko nchini ili iweze kupata picha halisi.

Naye kiongozi wa timu hiyo profesa Adele Jinadu alisema APRM ni mpango wa wakuu wan chi za Afrika ulioanzishwa mwaka 2002.


No comments:

Post a Comment