Wednesday, June 6, 2012

KILA KITU HUENDA MCHANGANUO NA MPANGO PIA

 Na Mwandishi wetu
Muleba
Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muleba wametakiwa kuhakikisha wanatoa mchanganuo kabla ya  kwenda ofisini kwa mhasibu mkuu wa Halmashauri hiyo kuomba pesa ya mafuta jambo ambalo imedaiwa kuwa itapunguza matumizi mabaya ya fedha ya Serikali na kuongeza pato la Halmashauri hiyo.
Tamko hilo limetolewa na mhasibu huyo Everist Shemdoe ambaye ni mgeni katika Halmashauri hiyo jana wakati wa kikao cha kawaida cha barza la madiwani cha  robo ya tatu ya mwaka kilichopfanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Halmashauri.
“Mimi na ahidi mbele ya kikao cha baraza la madiwani kuhakikisha sina urafiki na mtu kuhusu matumizi ya mabaya ya mafuta ya Serikali,nitahitaji kupewa mchanganuo  kwanza yatatumika katika shughuli gani namba ya gari na mengine ili nijilithishe ndipo nitatoa kibali cha mtu kuchukua mafuta katika kituo kilichopangwa na sio vinginevyo siwezi kukukubali mapato ya halmashauri ya kaendelaea kushuka  na kuendelea kushika mkia kati ya halmashauri za mkoa huu eti kwasababu ya matumizi makubwa katika eneo hili la mafuta kwani watanzania wa Muleba na Tanzania wanataka kuona pesa yao ya kodi inakuwa nathamani”alisema Shemdoe.
Alisema kuwakama watajitahidi kubana mianya ya matumizi ambayo hayana mpangilio na kuungana kwa pamoja kati ya madiwani na watendaji wakathibiti kikamilifu matumizi yasiyo ya lazima Halmashauri ya Muleba itapanda na kukamilisha lengo la makusudio yao.
 
Alisema kuwa kamati ya fedha uongozi na mipango ilipitia taarifa ya mapato na matumizi na kutoa maelekezo kuwa watumishi wote wanaohusika na ukusanyaji wa mapato wasikae ofisini badala yake wafanye kazi nje (field work) kwa ajili ya kukusanya mapato.
Alisema pia kamati hiyo ilipitia taarifa mbalimbali za kila idara na kujiridhisha juu ya matumizi hayo ambapo kamati hiyo imeendelea kuwaagiza wakuu wa idara kuzingatia kanuni za fedha wakati wa kufanya malipo hasa kwa kuzingatia vifungu vilivyoainishwa.
Pia kamati ilibaini kuwepo kwa madeni mbalimbali ya zabuni ya mialo pamoja na meza ambapo kwasasa upande wa mialo deni ilikuwa kiasi cha shilingi milioni 13.8 na deni la meza ni shilingi laki 8.3 ambapo kamati imetoa maelekezo kwamba madeni yote yakusanywe pale ambapo kuna utata basi sheria ichukue mkondo wakehata hivyo madeni maengine yale ya nyumba za watumishi yaliyoonekana kujirudia  na maelekezo ni kwamba kama mpangaji /mtumishi hataki kulipa basi aondoke kwenye nyumba za Halmashauri.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri hiyo GeorgeKatomelo alisema kuwa kwa kipindi cha miezi miwili tangu alipowasili mhasibu mkuu mpya Shemdoe kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi vijijini  ambapo kwasasa  halmashauri ya Muleba  imepanda kwa kiwango cha ukusanyaji mapato ukilinganisha na kipindi cha Januari mwaka huu Halmashauri hiyo ili kuwa ya Mwisho katika mawasilisho yaliyowasilishwa katika kikao cha ushauri cha mkoa ambapo ili pata asilimia 12 ya makusanyo huku Karagwe ikishika nafasi ya kwanza ambayo ilikusanya asilimia 98 na kwa sasa makusanyo ya Muleba yamepanda kutoka asilimia 12 hadi asilimia 62 ndani ya miezi miwili ambayo ni sawa na makusanyo ya shilingi bl.2 ukilinganisha na kiwango walichoamuliwa kukusanya cha shilingi bilioni 3.
Naye diwani wa kata ya Muleba Hassani Milanga aliishauri Halmashauri hiyo kuhakikisha inatunza na kuzilinda raslimalia za Halamashauri hiyo kwani ndizo zinazoongeza mapato yanayoiwezesha Halmashauri kusimamma na kuitwa Halmashauri.
 
Nao madiwani kwa nyakati tofauti wametoa tamko kwamba wanawapongeza watumishi wa Halmashauri hiyo kutokana na kiwango cha ukusanyajiwa mapato kupanda na kwa muda mfupi huku wakiwashauri kutorudi nuyma bali wendelee kukaza mwendo ili kuinusuru Halmashauri hiyo ambayo hushika mkia katika mambo ya maendeleo na ukusanyaji w amapato katika mkoa wa Kagera.

No comments:

Post a Comment