PICHA KUTOKA MAKTABA KKKT-KARAGWE DIOCESE
NA
JUHUDI FELIX-KARAGWE
Wakati mashirika na taasisi na wanaharakati kuwa katika harakati za kupinga ajira kwa watoto ambao wako chini ya umri wa miaka 18 kuajiriwa na kufanyishwa kazi nzito ambazo zinaleta athari katika maendeleo ya makuzi ya watoto hali ni tofauti na wilaya ya Karagwe mkoani Kagera kama picha inavyoonesha hapo juu.
Mashirika na taasisi zinazotetea unyanyasaji wa kijinsi sijui kama hali hii nao wanaichukuliaje imekuwa ni kawaida wasichana wa umri mdogo kufanyishwa kazi nzito majumbani na kufanyiwa vitendo vya kinyama ambavyo vinadhuru afya zao kimaendeleo pia kiafya serikali ,wadau na jamii kwa ujumla inabidi kuunganisha jitihada za pamoja katika kupinga ajira kwa watoto.
Hali ya kipato cha wazazi cha kumpeleka
mtoto wa kike shule inashindikana kiasi cha kumkatisha tamaa na kumfanya
ajiingize kwenye vishawishi vingine na hivyo ili kuondoa tatizo hili
katika jamii yetu ya Kitanzania,kunahitajika jitihada za pamoja za
Serikali,Taasisi mbali mbali na wadau wa Maendeleo wawe na dhamira ya
kweli na matumizi sahihi za raslimali zilizopo.
Serikali na wadau
wa maendeleo na jamii kwa ujumla inabidi kuwabaini watoto wa kike ambao
wako katika Mazingira hatarishi kwa sababu ya umaskini wa familia zao
wameshindwa kupata haki zao za msingi kama vile kupata elimu,ushirikishwaji katika mambo yanayowahusu hivyo na kuamua kujiingiza katika vitendo vya kuajiriwa kwa ajili ya kujipatia kipato cha kukidhi mahitaji yao ya msingi.
No comments:
Post a Comment